Loading...

Waziri Kitwanga Asema Wabunge Wataendelea Kukamatwa Kama Hawatafuata Sheria za Nchi.

> JE WEWE UNA ELIMU YA KIDATO CHA NNE ?PATA AJIRA NA UJIONGEZEE KIPATO HADI LAKI 8 KWA MWEZI WAHI NAFASI NI CHACHE BOFYA HAPA CHINI UPATE NAFASI..

JE WEWE UNA ELIMU YA KIDATO CHA NNE ?PATA AJIRA NA UJIONGEZEE KIPATO HADI LAKI 8 KWA MWEZI WAHI NAFASI NI CHACHE BOFYA HIYO PICHA HAPO JUU UPATE NAFASI.. ..LIKE PAGE !..



Wakati Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, akidai wabunge wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wanakamatwa bila sababu za msingi, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, amesema hakuna mtu anayekamatwa bila sababu na kwamba yeyote atakayebainika kufanya kosa, atasweka ndani bila kujali chama chake.

Machi Mosi, mwaka huu, Mbowe aliwaeleza waandishi wa habari kwamba wabunge na madiwani kutoka Ukawa, wanadhalilishwa na kunyanyaswa kila kona nchini na kwamba hizo ni juhudi za kurudisha nyuma maendeleo ya kazi za viongozi hao.

Hivi karibuni, Waziri Kitwanga alisema kuwa wananchi watambue kwamba askari polisi ni rafiki wa raia mwema, hivyo hawawezi kumkamata mtu asiyetenda kosa.

“Nitamshangaa askari polisi, mtu anatenda kosa pale wasimkamate eti kwa sababu tu ni mbunge wa upinzani. Awe wa CCM, awe wa upinzani watakamatwa, mimi nimeshawaeleza.

“Nimeshawaeleza wazi kabisa, mimi nitasimamia haki tu, tofauti na hapo hapana, wewe ungeona yule mama alivyopigwa na wabunge(Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando) inaumiza sana. Nilichukia sana lakini hata sikuwasemesha polisi, nilikaa kimiya tu niwaone watafanyaje.

“Niliamua kuwapima, ‘infact’ (kwa kweli) hawa watu hata dhamana wasingewapa kwa kitendo hicho,” alisema Kitwanga.
>
JISHINDIE SAMSUNG GALAXY MPYA KABISA JAZA FOMU NA UTAPIGIWA SIMU PAPO HAPO BOFYA HAPO JUU,RUDIA KUBOFYA MPAKA UONE SIMU UNAPIGIWA =>

Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by Lovetzz

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright WANAWAKE KWANZA | Modified By Zotekali WEB Exparts
Back To Top