JE WEWE UNA ELIMU YA KIDATO CHA NNE ?PATA AJIRA NA UJIONGEZEE KIPATO HADI LAKI 8 KWA MWEZI WAHI NAFASI NI CHACHE BOFYA HIYO PICHA HAPO JUU UPATE NAFASI.. ..LIKE PAGE !..
Mtoto Julias
Makoye (5) mkazi wa mwendakulima wilayani Kahama mkoani Shinyanga amenusurika
kifo mara baada ya kuchomwa moto na jirani yao Edina Peter 20, kwa tuhuma ya
kuiba simu na rimoti ya televisheni.
Mashuhuda wa
tukio hilo wameiambia Kahamafm kuwa tukio hilo limetokea juzi ambapo Edina amefanya
ukatili kwa mtoto Julias kwa kumwagia mafuta aina ya petrol mwili mzima na
kisha kumchoma moto uliomsababishia majeraha mwilini.
Mwenyekiti wa
mtaa wa mwendakulima kati Abrahamani Dulla, amefafanua kuwa mara baada ya Edina
kutekeleza tukio hilo walimchukua mtoto Julias bila kuwapa taarifa wazazi wake
na kumpeleka katika Zahanati ya Nyakato mjini Kahama.
Mama mzazi wa
mtoto huyo Ndalo Manyanda amesema mwanaye alikuwa anacheza katika nyumba ya
jirani na ghafla alipokea taarifa kutoka kwa majirani kuwa mwanaye amechomwa
moto kwa tuhuma ya kuiba simu na rimoti ya televisheni.
Amesema hali ya
mtoto wake inaendelea vizuri mara baada ya kupatiwa matibabu katika hospitali
ya halmashauri ya mji wa kahama huku akitoa rai kwa wasamaria wema kumsaidi
fedha ili mwanaye apatiwe matibabu.
Jeshi la polisi
wilayani kahama limetibitisha kutokea kwa tukio hilo na bado linaendelea
kuwashikilia Chalya Charles 30 na mkewe Edina
aliyedaiwa kufanya tukio hilo kwaajili ya upelelezi wa tukio hilo.
>
Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Facebook Plugin by Lovetzz


Post a Comment