Loading...

Zaidi ya bilioni 230/- zapotea kutokana na ajali barabarani.

> JE WEWE UNA ELIMU YA KIDATO CHA NNE ?PATA AJIRA NA UJIONGEZEE KIPATO HADI LAKI 8 KWA MWEZI WAHI NAFASI NI CHACHE BOFYA HAPA CHINI UPATE NAFASI..

JE WEWE UNA ELIMU YA KIDATO CHA NNE ?PATA AJIRA NA UJIONGEZEE KIPATO HADI LAKI 8 KWA MWEZI WAHI NAFASI NI CHACHE BOFYA HIYO PICHA HAPO JUU UPATE NAFASI.. ..LIKE PAGE !..



Serikali imesema zaidi ya Sh. bilioni 230 zimepotea katika kipindi cha mwaka uliopita kutokana na ajali za barabarani nchi nzima.
 
Akizungumza katika ufunguzi wa semina ya madereva wa magari makubwa, mabasi ya masafa marefu na daladala jijini Mwanza juzi, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Baraka Konisaga (pichani), alisema kiasi cha Sh. bilioni 230 zilipotea katika ajali zilizotokea kipindi hicho licha ya baadhi ya ajali hizo zingeweza kuepukika.
 
Katika semina hiyo ya kuwaelimisha madereva juu ya makosa ya kibinadamu yanavyochangia kwa kiasi kikubwa ajali za barabarani, Konisaga alisema uzembe, ulevi, uchakavu wa barabara, ubovu wa magari ni miongoni mwa sababu hizo.
 
“Katika kipindi cha mwaka jana pekee Sh. bilioni 230 zilipotea kutokana na matukio mbalimbali ya ajali za barabarani ambazo nyingi zimesababishwa na makosa ya binadamu,” alisema.
 
Awali akizungumza katika semina hiyo, Meneja wa Usalama Barabarani  na Mazingira wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchikavu (Sumatra), Geofrey Silanda, alisema tafiti mbalimbali zilizofanywa nchini zinaonyesha asilimia 75 za ajali za barabarani zinatokana na makosa ya kibinadamu.
 
“Lakini pia asilimia 50 ya makosa hayo ya barabarani yanayohusiana na mambo ya kibinadamu yanafanywa na madereva,” alisema Silanda.
 
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Madereva wa Mabasi Mkoani Mwanza (Uwamata), Shabani Wandiba, aliitupia lawama serikali kuwa ndiyo inayochangia kwa kiasi kikubwa kusababisha ajali za barabarani kutokana na kupanga muda wa magari kusafiri bila ya kuangalia umbali.
 
“Ratiba inapangwa bila kuangalia umbali, mwendo kulingana na alama za barabarani, mfano mwendo wa kilomita 80, 50, 20 kwa saa pamoja na muda wa chakula yote hayo ni miongoni mwa vyanzo vya ajali,” alisema Wandiba.
 
Naye Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Mwanza, Mrakibu wa Polisi Mohamed Likwata, alisema ajali nyingi zinasababishwa na madereva ambao wanashindwa kufuata sheria na alama za usalama barabarani kikamilifu.
 
Kuhusu muda, kamanda huyo alisema atashauriana na Sumatra kuangalia muda wa chakula wa dakika 10 ili uweze kuongezwa kutokana na mabasi yenye uwezo wa kuchukua abiria 60 kutoweza kutimiza sheria hiyo ambayo inawabana madereva.
>
JISHINDIE SAMSUNG GALAXY MPYA KABISA JAZA FOMU NA UTAPIGIWA SIMU PAPO HAPO BOFYA HAPO JUU,RUDIA KUBOFYA MPAKA UONE SIMU UNAPIGIWA =>

Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by Lovetzz

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright WANAWAKE KWANZA | Modified By Zotekali WEB Exparts
Back To Top