Loading...

Sheria ya Mtandao Yamtia Mbaroni Mtayarishaji wa Vipindi Mkoani Dodoma

> JE WEWE UNA ELIMU YA KIDATO CHA NNE ?PATA AJIRA NA UJIONGEZEE KIPATO HADI LAKI 8 KWA MWEZI WAHI NAFASI NI CHACHE BOFYA HAPA CHINI UPATE NAFASI..

JE WEWE UNA ELIMU YA KIDATO CHA NNE ?PATA AJIRA NA UJIONGEZEE KIPATO HADI LAKI 8 KWA MWEZI WAHI NAFASI NI CHACHE BOFYA HIYO PICHA HAPO JUU UPATE NAFASI.. ..LIKE PAGE !..


Mtayarishaji wa vipindi, Sospiter Jonas amefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo ya Dodoma Mjini akishtakiwa kwa matumizi mabaya ya mtandao.

Sospiter alisomewa mashtaka hayo na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Mussa mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo Emmanuel Bwile.

Mshtakiwa huyo anadaiwa kuandika katika ukurasa wake wa Facebook ujumbe kuwa “Pinda utakuwa muhubiri wa injili tu.”

Mussa aliiambia Mahakama kuwa mshtakiwa huyo alibandika picha ya John Maliga kwenye ukurasa wake wa Facebook na kuandika ujumbe huo, kitendo ambacho ni kinyume cha kifungu namba 16 cha Sheria ya Mtandao ya Mwaka 2015.

Mlalamikaji katika shauri hilo la jinai namba 815/2015 litakalokuja tena mahakamani Oktoba 19, ni John Maliga.

Mshtakiwa yupo nje baada ya kutimiza masharti ya dhamana iliyomtaka kuwa na mdhamini mmoja na bondi ya Sh1 milioni.

Kesi hii imekuja baada ya wiki iliyopita, kijana mmoja, Benedict Ngonyani (24) kufikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam akituhumiwa kusambaza taarifa za uongo zinazomhusu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Davis Mwamunyange.

Kijana huyo anatuhumiwa kuandika katika ukurasa wake wa Facebook na WhatsApp kuwa, Mwamunyange, amelazwa kwenye hospitali moja mjini Nairobi, Kenya kwa madai ya kulishwa chakula chenye sumu.
Mpekuzi blog 
>
JISHINDIE SAMSUNG GALAXY MPYA KABISA JAZA FOMU NA UTAPIGIWA SIMU PAPO HAPO BOFYA HAPO JUU,RUDIA KUBOFYA MPAKA UONE SIMU UNAPIGIWA =>

Asante! TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

Facebook Plugin by Lovetzz

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright WANAWAKE KWANZA | Modified By Zotekali WEB Exparts
Back To Top